Utitiri wa maduka ya dawa tatizo nchini KWA UFUPI Watu wanapata madhara kutokana na kukiukwa kwa taratibu za upatiwaji wa dawa unaofanyika zaidi katika maduka ya dawa yasiyo na wataalamu Dar es Salaam. Chama cha Mafamasia nchini (PST) kimesema matatizo mengi yatokanayo na matumizi mabaya ya dawa yanasababishwa na uwepo wa maduka ya dawa yasiyo na wataalamu na yanayoendeshwa kiholela . Akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Mafamasia nchini, Rais wa PST, Michael Kishua alisema Tanzania kama zilivyo nchi nyingine duniani, inaendeshwa kwa misingi na sheria katika huduma za dawa lakini kuna utekelezaji hafifu wa sheria. “Sisi kama chama, tukiona kuna upungufu tunazungumza na baraza la famasia ili warekebishe na mpaka sasa tumeona kuna mabadiliko makubwa kwa sababu hata sasa baraza la famasia lipo kazini likiangalia maduka yanayoendeshwa kiholela,” alisema Alisema tabia ya watu kununua dawa kiholela bila ya kuwa na cheti cha maelekezo daktari hufanywa na maduka ambayo ...
Comments
Post a Comment