Skip to main content

NATIONAL PHARMACY WEEK SUMMIT 20TH JUNE AT MNAZI MMOJA

Utitiri wa maduka ya dawa tatizo nchini
 KWA UFUPI Watu wanapata madhara kutokana na kukiukwa kwa taratibu za upatiwaji wa dawa unaofanyika zaidi katika maduka ya dawa yasiyo na wataalamu Dar es Salaam. Chama cha Mafamasia nchini (PST) kimesema matatizo mengi yatokanayo na matumizi mabaya ya dawa yanasababishwa na uwepo wa maduka ya dawa yasiyo na wataalamu na yanayoendeshwa kiholela

Akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Mafamasia nchini, Rais wa PST, Michael Kishua alisema Tanzania kama zilivyo nchi nyingine duniani, inaendeshwa kwa misingi na sheria katika huduma za dawa lakini kuna utekelezaji hafifu wa sheria. “Sisi kama chama, tukiona kuna upungufu tunazungumza na baraza la famasia ili warekebishe na mpaka sasa tumeona kuna mabadiliko makubwa kwa sababu hata sasa baraza la famasia lipo kazini likiangalia maduka yanayoendeshwa kiholela,” alisema Alisema tabia ya watu kununua dawa kiholela bila ya kuwa na cheti cha maelekezo daktari hufanywa na maduka ambayo yanavunja sheria na yale yasiyo na wataalamu na kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji. Kadhalika, chama hicho kilikiri kuwa yapo maduka yanayouza dawa za kutoa mimba na kusisitiza kuwa mienendo hiyo inakemewa kwa pamoja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Baraza la Mafamasia la Taifa. “Kigezo cha kwanza cha duka la dawa ni kusajiliwa na kuwa na wataalamu wa masuala ya dawa. Baraza la Mafamasia haliwezi kusajili duka bila kuwa na mtaalamu wa uhakika,” alisema Kishua. Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa PST, Elias Masumbuko alisema ipo sheria inayofafanua dawa zinazotakiwa kununuliwa bila cheti na zile za moto zinazohitaji cheti lakini mara kadhaa sheria hiyo inakiukwa. Aliwataka wamiliki wa maduka ya dawa kutoweka mbele biashara badala yake wazingatie maadili ya taaluma ili kuepusha madhara. Wakizungumzia maadhimisho ya wiki hiyo ya mafamasia nchini inayofikia kilele chake leo, Kishua alisema ni vyema Watanzania wakaeleweshwa umuhimu wa kupata dawa kwenye vyanzo vinavyoaminika na salama. Alisema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo ni Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donald Mbando ambaye pia atazindua tovuti ya chama hicho. Maadhimsho ya Wiki ya Mafamasia nchini kwa mwaka huu yanapambwa na kauli mbiu isemayo, ‘Elewa dawa zako, mfahamu famasia wako.’   








                           





























Comments

Popular posts from this blog

THE OFFICE OF THE CHAIRPERSON MUHAS MID BUSINESS REPORT 2015/2016

INTRODUCTION Tanzania Pharmaceutical Students’ Association is a national wise association with a full membership of the International Pharmaceutical Students’ Federation (IPSF). Currently the association comprises six branches, namely Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS), St. Johns University of Tanzania (SJUT), Catholic University of Health and Allied Sciences (CUHAS), Ruaha Catholic University (RUCU), University of Dodoma (UDOM) and currently Kilimanjaro International University (KIU) with about 1500 TAPSA members who actively participate in various activities organized by the association. As MUHAS branch we assumed our positions at the end of May 2015 after general election and only a year term. SOURCES OF FUNDS Most sources of funds are student fees, some projects like T-Shirts, TAPSA stationary, Fund raising and Donors.   ACTIVITIES OF THE ASSOCIATION IN THE YEAR 2015 Education and Practice Activities Within association we managed to conduct various tr...

NO LONGER A MYTH: Octopus Soup Boosts Libido

  It is not a myth anymore. We now have the preliminary evidence that gives us a ray of hope to prove the same in humans. Octopus soup—supu ya pweza—can indeed boost sexual desire in men.  However, Professor Kaale is quick to warn octopus soup consumers that the new findings doesn’t mean that a cure for sexual dysfunction among men has been found. Pharmacists at Muhimbili University of Health and Allied Sciences (Muhas) say they now have scientific proof that octopus soup—popular known as supu ya pweza—can indeed boost sexual desire in men. For many years, it was widely believed by most people living along the coast of Tanzania and the wider East Africa that octopus soup increases libido among men. But there was no scientific evidence to back up their claims. “It should not be a myth anymore. We now have the preliminary evidence that gives us a ray of hope to prove the same effect in humans in further studies,” says Professor Eliangiringa Kaale, the Head of the Research...

ADDO PROGRAM. Accredited Drug Dispensing Outlets in Tanzania

In the past,   duka la dawa baridi in Tanzania were authorized to sell nonprescription medicines. However, a 2001 assessment showed that many shops sold prescription drugs illegally and that the drug sellers were generally unqualified and untrained. In response, the Tanzania Food and Drugs Authority (TFDA) worked with Management Sciences for Health (MSH) to develop and launch the accredited drug dispensing outlet (ADDO) program—or   Duka la Dawa Muhimu —in 2003 in Ruvuma region. The goal of the ADDO program was to improve access to affordable, quality medicines and pharmaceutical services in areas where few or no registered pharmacies existed. The program’s primary activities include— Developing accreditation based on Ministry of Health and Social Welfare-instituted standards and regulations Creating a strong public sector-based regulatory and inspection system and strengthening local regulatory processes and capacity Developing drug shop owners’ business skills ...