Skip to main content

NATIONAL PHARMACY WEEK SUMMIT 20TH JUNE AT MNAZI MMOJA

Utitiri wa maduka ya dawa tatizo nchini
 KWA UFUPI Watu wanapata madhara kutokana na kukiukwa kwa taratibu za upatiwaji wa dawa unaofanyika zaidi katika maduka ya dawa yasiyo na wataalamu Dar es Salaam. Chama cha Mafamasia nchini (PST) kimesema matatizo mengi yatokanayo na matumizi mabaya ya dawa yanasababishwa na uwepo wa maduka ya dawa yasiyo na wataalamu na yanayoendeshwa kiholela

Akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Mafamasia nchini, Rais wa PST, Michael Kishua alisema Tanzania kama zilivyo nchi nyingine duniani, inaendeshwa kwa misingi na sheria katika huduma za dawa lakini kuna utekelezaji hafifu wa sheria. “Sisi kama chama, tukiona kuna upungufu tunazungumza na baraza la famasia ili warekebishe na mpaka sasa tumeona kuna mabadiliko makubwa kwa sababu hata sasa baraza la famasia lipo kazini likiangalia maduka yanayoendeshwa kiholela,” alisema Alisema tabia ya watu kununua dawa kiholela bila ya kuwa na cheti cha maelekezo daktari hufanywa na maduka ambayo yanavunja sheria na yale yasiyo na wataalamu na kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji. Kadhalika, chama hicho kilikiri kuwa yapo maduka yanayouza dawa za kutoa mimba na kusisitiza kuwa mienendo hiyo inakemewa kwa pamoja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Baraza la Mafamasia la Taifa. “Kigezo cha kwanza cha duka la dawa ni kusajiliwa na kuwa na wataalamu wa masuala ya dawa. Baraza la Mafamasia haliwezi kusajili duka bila kuwa na mtaalamu wa uhakika,” alisema Kishua. Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa PST, Elias Masumbuko alisema ipo sheria inayofafanua dawa zinazotakiwa kununuliwa bila cheti na zile za moto zinazohitaji cheti lakini mara kadhaa sheria hiyo inakiukwa. Aliwataka wamiliki wa maduka ya dawa kutoweka mbele biashara badala yake wazingatie maadili ya taaluma ili kuepusha madhara. Wakizungumzia maadhimisho ya wiki hiyo ya mafamasia nchini inayofikia kilele chake leo, Kishua alisema ni vyema Watanzania wakaeleweshwa umuhimu wa kupata dawa kwenye vyanzo vinavyoaminika na salama. Alisema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo ni Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donald Mbando ambaye pia atazindua tovuti ya chama hicho. Maadhimsho ya Wiki ya Mafamasia nchini kwa mwaka huu yanapambwa na kauli mbiu isemayo, ‘Elewa dawa zako, mfahamu famasia wako.’   








                           





























Comments

Popular posts from this blog

REPORT ON CAREER PATH EVENT HELD ON 3rd AUGUST

       Career path event, an annual function organized by TAPSA-MUHAS in cooperation with the school of pharmacy, this year was held on the 3 rd of August, 2018 at Muhimbili University of Health and Allied Sciences, lecture hall 5 from 12:30hrs to 17:00hrs.        The purpose of this event was to ensure that the students never lose motivation along the way of their studies and to assist students in developing goals to strive for and to be able to make major career decisions. Furthermore, to allow a panel of motivational speakers to share their stories with the students, with the goal of giving them more clarity about different career paths.       With positive attitude and true motivation, the event this year was convened by Prof. Dr. E. Kaale (Head,Pharmaceutical Analysis Lab,Pharmaceutical R&D laboratory in School of Pharmacy) and the panelists were as follows;   ...

ABOUT TAPSA

Being the student aspiring to be health cadre delivers and service providers we are entitled responsibility to the Tanzanians and world at large as tomorrow health practitioners. Having a goal to prepare diligent health professionals ADUPS was founded in Mid August 1987 by MUCHS pharmacy students and as a result of guidance and support from IPSF, the association was officially registered on the 4th April 1990 in UDSM.  It became a full member of IPSF and APSF in August 1993 and September 2002 respectively.  ADUPS has being active for almost twenty years and her members have every reason to be proud for attaining this age. In the year-2007 MUCHS declared transformation from being a constituent College of University of Dar es Salaam to full fledged University hereby namely MUHAS. ADUPS had to transform her name and become TAPSA.  Following this expansion the association is having chapters in Colleges/Universities providing a bachelor of P...

CAREER PATH EVENT - 3rd AUGUST 2018 (Photos)