Skip to main content

KUFUTA USAJILI NA KUDHIBITI MATUMIZI YA BAADHI YA DAWA ZA BINADAMU



MAMLAKA YA CHAKULA NA DAWA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


KUFUTA USAJILI NA KUDHIBITI MATUMIZI YA BAADHI YA DAWA ZA BINADAMU


1.    Mamlaka ya Chakula na Dawa ni wakala wa Serikali chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yenye jukumu la kudhibiti usalama, ubora na ufanisi wa chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba.

2.    Mamlaka imeweka mifumo mbalimbali ya udhibiti ikiwa ni pamoja na mifumo ya tathmini na usajili, ukaguzi, uchunguzi wa kimaabara, ufuatiliaji wa usalama wa dawa (pharmacovigilance) na ufuatiliaji wa ubora wa dawa kwenye soko (post-marketing surveillance).

3.    Mamlaka inapenda kuutaarifu umma kuwa kupitia mifumo ya ufuatiliaji wa usalama na ubora wa dawa imebaini uwepo wa dawa duni kwenye soko, zenye madhara na zisizofaa kwa matumizi ya binadamu.

4.    Kufuatia hali hiyo, Mamlaka imefuta usajili wa aina tano (5) za dawa za binadamu  kama ifuatavyo:-

Na.
Aina ya Dawa
Hatua iliyochukuliwa
Sababu za kuchukua hatua
i.
Dawa ya kutibu “fungus” ya vidonge na kapsuli aina ya Ketoconazole
Kufuta usajili na kuzuia uingizaji, usambazaji, uuzaji na matumizi
Kusababisha madhara hatarishi katika ini kwa watumiaji (liver toxicity)
ii.
Dawa ya kutibu malaria ya maji na vidonge aina ya Amodiaquine (Monotherapy)
Kufuta usajili na kuzuia uingizaji, usambazaji, uuzaji na matumizi

·         Mabadiliko ya Mwongozo wa Kisera wa Kupima na Kutibu Malaria wa mwaka 2013, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
·         Amodiaquine ikitumika peke yake (monotherapy) inaleta usugu wa  vimelea vya malaria lakini  itaendelea kutumika kama dawa ya mseto pamoja na “Artesunate”.
iii.
Dawa za kutibu mafua na kikohozi za maji, vidonge na kapsuli zenye kiambato hai aina ya Phenylpropanolamine

Kufuta usajili na kuzuia uingizaji, usambazaji, uuzaji na matumizi
Madhara hatarishi kwa watumiaji kama vile kiharusi (hemorrhagic stroke)
iv.
Dawa ya kuua bakteria ya sindano aina ya Chloramphenicol Sodium Succinate inayotengenezwana kiwanda cha Lincoln Pharmaceuticals Ltd, India
·      Kufuta usajili na kuzuia uingizaji, usambazaji, uuzaji na matumizi

·      Dawa zenye kiambata hai aina ya Chloramphenicol za makampuni mengine zinafanyiwa tathmini na ikibainika zina madhara zitaondolewa kwenye soko.

Madhara hatarishi kwa watumiaji kama vile kushindwa kupumua na kupoteza fahamu (difficulty in breathing and loss of consciousness)
v.
Dawa ya kuua bakteria ya maji na kapsuli aina ya Cloxacillin
·      Kufuta usajili na kuzuia uingizaji

·      Dawa hii imeanza kuondolewa kwenye soko (phasing out)
Kiwango cha  kiambato hai hupungua kabla ya muda wa matumizi kumalizika (loss of potency before expiry date)

5.    Vile vile, Mamlaka imebadili na kudhibiti zaidi matumizi ya dawa nne (4) kama ifuatavyo:-

Na
Aina ya Dawa
Hatua iliyochukuliwa
Sababu za kuchukua hatua
i.
Dawa ya kutibu malaria ya vidonge yenye mchanganyiko wa Sulphadoxine na Pyrimethamine(SP)
·       Kubadili matumizi kutoka tiba ya malaria na kuwa kinga ya malaria kwa kinamama wajawazito

·       Watengenezaji wamejulishwa na wamebadili lebo za dawa hizo


Mabadiliko ya Mwongozo wa kisera wa Kupima na Kutibu Malaria wa mwaka 2013, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii

ii.
Dawa aina ya Kanamycin, Amikacin na Levofloxacin
Kudhibiti matumizi kwa kuruhusu dawa hizi kutumika kwa ajili ya ugonjwa wa kifua kikuu katika hospitali, vituo vya afya na zahanati tu
Kuzuia usugu wa vimelea vya bakteria
vya ugonjwa wa kifua kikuu

6.    Kutokana na maamuzi haya, Mamlaka inatoa maelekezo yafuatayo kwa watoa huduma za afya:

a.            Kuacha kutoa kwa wagonjwa dawa zilizofutiwa usajili yaani Ketoconazole, Amodiaquine (inapotumika yenyewe - monotherapy), Phenylpropanolamine na Chloramphenicol Succinate Injection ya Lincoln Pharmaceuticals Ltd., India na badala yake wazirudishe kwa wasambazaji wa dawa hizo.

b.            Kusimamia mabadiliko ya matumizi ya dawa aina ya SP ili ziweze kutumika kwa kinamama wajawazito tu na dawa aina ya Kanamycin, Amikacin na Levofloxacin  zitumike kwa wagonjwa wa kifua kikuu tu kwenye hospitali, vituo vya afya na zahanati.

c.            Kuendelea  kutoa dawa aina ya Cloxacillin hadi hapo itakapomalizika kwenye soko kwa sababu matoleo (batches) yaliyopo yameshapimwa na kuthibitishwa kuwa yanakidhi vigezo vya ubora.

7.    Tunawahakikishia watoa huduma za afya na wananchi kwamba kuondolewa katika soko kwa dawa zilizofutiwa usajili hakutaathiri tiba kwa kuwa zipo dawa mbadala zinazoweza kutibu magonjwa yanayotibiwa na dawa hizi.

8.    Tunawakumbusha watengenezaji na wasambazaji wa dawa kuhakikisha kwamba wanatengeneza dawa zinazokidhi vigezo vya  usalama, ubora na ufanisi kwa mujibu wa Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi, Sura 219.  Wale wote watakaobainika kuingiza na kusambaza dawa zilizofutiwa usajili watachukuliwa hatua kali za kisheria.

9.    Tunawashukuru watalaam wa afya na wananchi kwa ujumla kwa kuendelea kutoa taarifa za madhara na ubora wa dawa zilizo kwenye soko kwani kwa kufanya hivyo wananchi watajikinga na madhara yatokanayo na matumizi ya dawa na kuwa na afya njema.

10.  Tunawashukuru wanahabari kwa ushirikiano mkubwa ambao mmekuwa mkiuonesha katika kutoa taarifa zinazohusu masuala ya udhibiti wa ubora na usalama wa chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba na tunaomba muendeleze ushirikiano huo.






Imetolewa na;

Mkurugenzi Mkuu,
Mamlaka ya Chakula na Dawa,
S.L.P 77150,
  Dar es Salaam.
Simu: +255 22 2452108/2450512/2450751/658 445222/777 700 002
Nukushi: +255 22 2450793
Baruapepe: info@tfda.or.tz

Comments

Popular posts from this blog

THE OFFICE OF THE CHAIRPERSON MUHAS MID BUSINESS REPORT 2015/2016

INTRODUCTION Tanzania Pharmaceutical Students’ Association is a national wise association with a full membership of the International Pharmaceutical Students’ Federation (IPSF). Currently the association comprises six branches, namely Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS), St. Johns University of Tanzania (SJUT), Catholic University of Health and Allied Sciences (CUHAS), Ruaha Catholic University (RUCU), University of Dodoma (UDOM) and currently Kilimanjaro International University (KIU) with about 1500 TAPSA members who actively participate in various activities organized by the association. As MUHAS branch we assumed our positions at the end of May 2015 after general election and only a year term. SOURCES OF FUNDS Most sources of funds are student fees, some projects like T-Shirts, TAPSA stationary, Fund raising and Donors.   ACTIVITIES OF THE ASSOCIATION IN THE YEAR 2015 Education and Practice Activities Within association we managed to conduct various tr...

NO LONGER A MYTH: Octopus Soup Boosts Libido

  It is not a myth anymore. We now have the preliminary evidence that gives us a ray of hope to prove the same in humans. Octopus soup—supu ya pweza—can indeed boost sexual desire in men.  However, Professor Kaale is quick to warn octopus soup consumers that the new findings doesn’t mean that a cure for sexual dysfunction among men has been found. Pharmacists at Muhimbili University of Health and Allied Sciences (Muhas) say they now have scientific proof that octopus soup—popular known as supu ya pweza—can indeed boost sexual desire in men. For many years, it was widely believed by most people living along the coast of Tanzania and the wider East Africa that octopus soup increases libido among men. But there was no scientific evidence to back up their claims. “It should not be a myth anymore. We now have the preliminary evidence that gives us a ray of hope to prove the same effect in humans in further studies,” says Professor Eliangiringa Kaale, the Head of the Research...

ADDO PROGRAM. Accredited Drug Dispensing Outlets in Tanzania

In the past,   duka la dawa baridi in Tanzania were authorized to sell nonprescription medicines. However, a 2001 assessment showed that many shops sold prescription drugs illegally and that the drug sellers were generally unqualified and untrained. In response, the Tanzania Food and Drugs Authority (TFDA) worked with Management Sciences for Health (MSH) to develop and launch the accredited drug dispensing outlet (ADDO) program—or   Duka la Dawa Muhimu —in 2003 in Ruvuma region. The goal of the ADDO program was to improve access to affordable, quality medicines and pharmaceutical services in areas where few or no registered pharmacies existed. The program’s primary activities include— Developing accreditation based on Ministry of Health and Social Welfare-instituted standards and regulations Creating a strong public sector-based regulatory and inspection system and strengthening local regulatory processes and capacity Developing drug shop owners’ business skills ...