Skip to main content

NATIONAL PHARMACY WEEK SUMMIT 20TH JUNE AT MNAZI MMOJA

Utitiri wa maduka ya dawa tatizo nchini
 KWA UFUPI Watu wanapata madhara kutokana na kukiukwa kwa taratibu za upatiwaji wa dawa unaofanyika zaidi katika maduka ya dawa yasiyo na wataalamu Dar es Salaam. Chama cha Mafamasia nchini (PST) kimesema matatizo mengi yatokanayo na matumizi mabaya ya dawa yanasababishwa na uwepo wa maduka ya dawa yasiyo na wataalamu na yanayoendeshwa kiholela

Akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Mafamasia nchini, Rais wa PST, Michael Kishua alisema Tanzania kama zilivyo nchi nyingine duniani, inaendeshwa kwa misingi na sheria katika huduma za dawa lakini kuna utekelezaji hafifu wa sheria. “Sisi kama chama, tukiona kuna upungufu tunazungumza na baraza la famasia ili warekebishe na mpaka sasa tumeona kuna mabadiliko makubwa kwa sababu hata sasa baraza la famasia lipo kazini likiangalia maduka yanayoendeshwa kiholela,” alisema Alisema tabia ya watu kununua dawa kiholela bila ya kuwa na cheti cha maelekezo daktari hufanywa na maduka ambayo yanavunja sheria na yale yasiyo na wataalamu na kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji. Kadhalika, chama hicho kilikiri kuwa yapo maduka yanayouza dawa za kutoa mimba na kusisitiza kuwa mienendo hiyo inakemewa kwa pamoja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Baraza la Mafamasia la Taifa. “Kigezo cha kwanza cha duka la dawa ni kusajiliwa na kuwa na wataalamu wa masuala ya dawa. Baraza la Mafamasia haliwezi kusajili duka bila kuwa na mtaalamu wa uhakika,” alisema Kishua. Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa PST, Elias Masumbuko alisema ipo sheria inayofafanua dawa zinazotakiwa kununuliwa bila cheti na zile za moto zinazohitaji cheti lakini mara kadhaa sheria hiyo inakiukwa. Aliwataka wamiliki wa maduka ya dawa kutoweka mbele biashara badala yake wazingatie maadili ya taaluma ili kuepusha madhara. Wakizungumzia maadhimisho ya wiki hiyo ya mafamasia nchini inayofikia kilele chake leo, Kishua alisema ni vyema Watanzania wakaeleweshwa umuhimu wa kupata dawa kwenye vyanzo vinavyoaminika na salama. Alisema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo ni Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donald Mbando ambaye pia atazindua tovuti ya chama hicho. Maadhimsho ya Wiki ya Mafamasia nchini kwa mwaka huu yanapambwa na kauli mbiu isemayo, ‘Elewa dawa zako, mfahamu famasia wako.’   








                           





























Comments

Popular posts from this blog

ABOUT TAPSA

Being the student aspiring to be health cadre delivers and service providers we are entitled responsibility to the Tanzanians and world at large as tomorrow health practitioners. Having a goal to prepare diligent health professionals ADUPS was founded in Mid August 1987 by MUCHS pharmacy students and as a result of guidance and support from IPSF, the association was officially registered on the 4th April 1990 in UDSM.  It became a full member of IPSF and APSF in August 1993 and September 2002 respectively.  ADUPS has being active for almost twenty years and her members have every reason to be proud for attaining this age. In the year-2007 MUCHS declared transformation from being a constituent College of University of Dar es Salaam to full fledged University hereby namely MUHAS. ADUPS had to transform her name and become TAPSA.  Following this expansion the association is having chapters in Colleges/Universities providing a bachelor of P...

2015/2016 THE EXECUTIVE OFFICIALS AND TAPSA STANDING COMMITTEE

For the year 2015/2016 the executive officials are The President -   JOEL JOSEPH LUMENDE Vice President -   MGAMBI G GAMBA General Secretary -   GRACE FAUSTINE Treasure - Joel Kibona publicity officer   -Anania Anangise   TAPSA STANDING COMMITTEE 2015-2016 1. STANDING COMMITTEE ON ACADEMICS 1) CALVIN ANDREA            BPHARM 3  {councilor}  2) HERRY WAGI                    BPHARM 1  {vice councilor} 3) HAPPY RUPAMBA           BPHARM 2  { secretary}  4) DISMAS  MAKAMBA       DPS  2          {coordinator} 2. STANDING COMMITTEE ON PHARMACEUTICAL PROMOTION  1) DOMITILA JACOB         BPHARM 1  {councilor} 2)  JOHN PAUL HIRARY    DPS 1           { vice councilor} 3) ...

WHAT OCCURED ON SCIENTIFIC CONFERENCE PRE-EXPOSITION EVENT

 Mr President JOEL JOSEPH RUMENDE  addressing the key issues pertaining to scientific conference   members listening careful to organization committee of scientific conference