Skip to main content

NATIONAL PHARMACY WEEK SUMMIT 20TH JUNE AT MNAZI MMOJA

Utitiri wa maduka ya dawa tatizo nchini
 KWA UFUPI Watu wanapata madhara kutokana na kukiukwa kwa taratibu za upatiwaji wa dawa unaofanyika zaidi katika maduka ya dawa yasiyo na wataalamu Dar es Salaam. Chama cha Mafamasia nchini (PST) kimesema matatizo mengi yatokanayo na matumizi mabaya ya dawa yanasababishwa na uwepo wa maduka ya dawa yasiyo na wataalamu na yanayoendeshwa kiholela

Akizungumza katika maadhimisho ya Wiki ya Mafamasia nchini, Rais wa PST, Michael Kishua alisema Tanzania kama zilivyo nchi nyingine duniani, inaendeshwa kwa misingi na sheria katika huduma za dawa lakini kuna utekelezaji hafifu wa sheria. “Sisi kama chama, tukiona kuna upungufu tunazungumza na baraza la famasia ili warekebishe na mpaka sasa tumeona kuna mabadiliko makubwa kwa sababu hata sasa baraza la famasia lipo kazini likiangalia maduka yanayoendeshwa kiholela,” alisema Alisema tabia ya watu kununua dawa kiholela bila ya kuwa na cheti cha maelekezo daktari hufanywa na maduka ambayo yanavunja sheria na yale yasiyo na wataalamu na kusababisha madhara makubwa kwa watumiaji. Kadhalika, chama hicho kilikiri kuwa yapo maduka yanayouza dawa za kutoa mimba na kusisitiza kuwa mienendo hiyo inakemewa kwa pamoja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Baraza la Mafamasia la Taifa. “Kigezo cha kwanza cha duka la dawa ni kusajiliwa na kuwa na wataalamu wa masuala ya dawa. Baraza la Mafamasia haliwezi kusajili duka bila kuwa na mtaalamu wa uhakika,” alisema Kishua. Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa PST, Elias Masumbuko alisema ipo sheria inayofafanua dawa zinazotakiwa kununuliwa bila cheti na zile za moto zinazohitaji cheti lakini mara kadhaa sheria hiyo inakiukwa. Aliwataka wamiliki wa maduka ya dawa kutoweka mbele biashara badala yake wazingatie maadili ya taaluma ili kuepusha madhara. Wakizungumzia maadhimisho ya wiki hiyo ya mafamasia nchini inayofikia kilele chake leo, Kishua alisema ni vyema Watanzania wakaeleweshwa umuhimu wa kupata dawa kwenye vyanzo vinavyoaminika na salama. Alisema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho hayo ni Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donald Mbando ambaye pia atazindua tovuti ya chama hicho. Maadhimsho ya Wiki ya Mafamasia nchini kwa mwaka huu yanapambwa na kauli mbiu isemayo, ‘Elewa dawa zako, mfahamu famasia wako.’   








                           





























Comments

Popular posts from this blog

THE OFFICE OF THE CHAIRPERSON MUHAS MID BUSINESS REPORT 2015/2016

INTRODUCTION Tanzania Pharmaceutical Students’ Association is a national wise association with a full membership of the International Pharmaceutical Students’ Federation (IPSF). Currently the association comprises six branches, namely Muhimbili University of Health and Allied Sciences (MUHAS), St. Johns University of Tanzania (SJUT), Catholic University of Health and Allied Sciences (CUHAS), Ruaha Catholic University (RUCU), University of Dodoma (UDOM) and currently Kilimanjaro International University (KIU) with about 1500 TAPSA members who actively participate in various activities organized by the association. As MUHAS branch we assumed our positions at the end of May 2015 after general election and only a year term. SOURCES OF FUNDS Most sources of funds are student fees, some projects like T-Shirts, TAPSA stationary, Fund raising and Donors.   ACTIVITIES OF THE ASSOCIATION IN THE YEAR 2015 Education and Practice Activities Within association we managed to conduct various tr...

2015/2016 THE EXECUTIVE OFFICIALS AND TAPSA STANDING COMMITTEE

For the year 2015/2016 the executive officials are The President -   JOEL JOSEPH LUMENDE Vice President -   MGAMBI G GAMBA General Secretary -   GRACE FAUSTINE Treasure - Joel Kibona publicity officer   -Anania Anangise   TAPSA STANDING COMMITTEE 2015-2016 1. STANDING COMMITTEE ON ACADEMICS 1) CALVIN ANDREA            BPHARM 3  {councilor}  2) HERRY WAGI                    BPHARM 1  {vice councilor} 3) HAPPY RUPAMBA           BPHARM 2  { secretary}  4) DISMAS  MAKAMBA       DPS  2          {coordinator} 2. STANDING COMMITTEE ON PHARMACEUTICAL PROMOTION  1) DOMITILA JACOB         BPHARM 1  {councilor} 2)  JOHN PAUL HIRARY    DPS 1           { vice councilor} 3) ...

WHAT OCCURED ON SCIENTIFIC CONFERENCE PRE-EXPOSITION EVENT

 Mr President JOEL JOSEPH RUMENDE  addressing the key issues pertaining to scientific conference   members listening careful to organization committee of scientific conference